September 27, 2010

Ushauri kutoka kwa Afande!

"Mambo vp kaka? Maoni yangu leo kama mpiga kura, mzalendo na msanii mkubwa ni haya hapa. Viongozi wa dini wasikimbilie kwa MUNGU kuomba amani wakati huu wa uchaguzi bali wanatakiwa wawaambie Tume ya Uchaguzi
wasijaribu kuchezea kura za watu kwa kutaka kumbeba mtu au chama chochote mahali ambapo hakikubaliki.



Wakifanya hivyo mwaka huu nina hakika amani itavunjika wala maombi kwa MUNGU hayatasaidia na bilashaka itakuwa kama Kenya, kitu ambacho kitafanya viongozi wa Tume ya Uchaguzi na wa Serikali wakutanena mkono wa sheria katika Mahakama ya Kimataifa 'The Heque' chini ya Moreno Ocampo.

Siyo kila jambo Wa-TZ tumsingizie MUNGU au shetani wakati tunasababisha wenyewe kwa tamaa zaUFISADI wa baadhi ya watu. Tukifanya uchaguzi huru na wa haki daima huwa na amani lakini wizi wa kura, udanganyifu na kuchakachua matokeo ndiyo sababu kubwa ya vita, uasi na matatizo katika taifa lolote"

No comments:

Post a Comment