October 12, 2010

Alicia Keys Na Mumewe Pamoja Na Usher Waieleza Jamii Kuhusu Kampeni Ya "Nunua Maisha":

Mama Swizz Beatz a.k.a Alicia Keys Ameanzisha Kampeni Ya Nunua Maisha Yenye Lengo La Kuwasaidia Watoto wasiojiweza Kutoka barani Afrika na India kupitia kampeni ya Waache Watoto Hai. Na Tayari Rafiki zake wameonesha Nia Ya Kusapoti Akiwemo Usher Raymond.

New York native songstress Alicia Keys Anaetarajia Kujifungua mtoto wa kwanza kutoka kwa mumewe mpya Produza mkali wa maeffect Swizz Beatz Mmiliki wa Studio Za J Records ambazo Keys Anafanyia Kazi, akiwa na mawazo kibao ya ujio wa mtoto wake Alicia keys ameanza kufanya mapambano juu ya kampeni hiyo ya "mwache mtoto hai" Mumewe Swizz nae hayuko mbali naye huku wakali wenzie Usher na Jay Sean wakionekana katika kampeni pacha ya Nunua Maisha itakayosimamiwa nae Keys na Swizz.

Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha kiss fm ya marekani Ryan Seacrest na mwanamitindo Kim Kardashan nao wamesaini kumpa support Alicia Keys ambaye ameamua kutengeneza nguo zitakazokuwa na brand ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasaidia watu waishio na HIV na Ukimwi Kutoka Barani Afrika na India.

"Katika uzinduzi wa kampeni ya "NUNUA MAISHA", Naamini kuwa watu wengi watapata msaada na kuepukana na tatizo la kufa kwa kukosa huduma muhimu za afya"

Meseji ya uchangiaji kwa njia ya simu itasaidia katika upatikanaji wa chakula, mavazi na madawa, Kushiriki katika kampeni hiyo ya kusaidia wasiojiweza andika neno "Alicia acha nafasi kisha tuma kwenda 90999.

No comments:

Post a Comment