November 27, 2011

Jeshi La Polisi Kenya Lawaomba Radhi Wananchi Wake.

Juzi kwenye eneo la kawangware kwenye jiji la Nairobi kulikua kwa moto baada ya maandamano ya maelfu ya watu, yaliyopelekea mambo mengi kusimamishwa kama usafiri na biashara, maandamano yaliyofanywa na wakazi wa eneo hilo kutokana na kulaumu mauaji ya baba na mtoto wake wa miaka 14, ambao inaaminika wameuwawa na polisi kimakosa.


Kibuchi ambae ni mkuu wa polisi Nairobi, amesema askari wote waliohusika na kosa hilo wamefutwa kazi na jana wamepandishwa mahakamani, ambapo pia mkuu huyo wa polisi ameomba radhi kwa kitendo walichofanya askari wake.

No comments:

Post a Comment