October 19, 2010

Ms. Triniti kuirusha Tz!:

Kupitia kwa wakali wawili wa muziki wa Bongo Fleva, Ambwene Yesaya ‘A.Y’ na Ilunga Kharifa ‘Cpwaa’ upo uwezekano mkubwa kwa mwanadada Ms. Triniti mwenye asili ya Trinidadi na Amerika
kuipeperusha Bongo mbali zaidi.

Kauli hiyo ilithibishwa na A.Y alipokuwa akigonga ishu mbili tatu na kusema kolabo aliyofanya na staa huyo wa kimataifa huenda ikazaa matunda kwa wasanii wa Bongo kupata dili nyingi katika nchi za mbali.

“Nimefanya naye ngoma yenye jina la ‘Goog Look’ ambayo video yake tumepiga Uganda, naamini ataipeleka mbali zaidi na kutufanya Wabongo tutambulike kimataifa,” alisema Ambwene.

Msanii mwingine aliyepiga kolabo na Ms. Triniti aliyekuja Bongo hivi karibuni kwa ajili ya shoo kadhaa ni ‘Cpwaa’.

No comments:

Post a Comment